Diese Publication Issue nicht in Ihrer Sprache vorhanden, Sehen Sie in: Kiswahili (sw),
Nutzen Sie die Google Übersetzen:  

Karanga ni mojawapo ya mazao yanayotoa mafuta. Katika Tanzania zao hili hustawi zaidi katika mikoa ya Kusini Mashariki, Dodoma na Morogoro. Pamoja na kutoa mafuta vile vile zao hutumika kwa njia nyingine mbali mbali, nazo ni pamoja na: Chakula cha wanyama / mifugo (Mashudu na majani), kurutubisha ardhi na chakula cha binadamu: kutafuna na kuunga kwenye mboga/chakula. Kwa ujumla zao hili hutumika na wakulima kama zao la biashara.